Mpaka Mapumziko timu hizo zilishafungana bao 1-1 Thembinkosi Lorch kutangulia kuipatia Pirates bao la kwanza kabla ya Leonardo Castro hajaisawazishia Chiefs.
Kipindi cha Pili Orlando Pirates walionekana kuimarika zaidi na kufanikiwa kupata mabao mawili yote yakifungwa na Amigo Memela.
Matokeo haya yanaifanya Orlando Pirates kufikisha pointi 39 katika nafasi ya pili wakiwa point 4 nyuma ya Vinara Mamelodi Sundowns wakati Kaizer Chiefs wao wanabaki na pointi zao 35 katika nafasi ya tatu.
Comments